Saturday, April 16, 2016


Image result for KUCHIMBA MAFUTA
Wawakilishi wa nchi zinazozalisha mafuta kwa wingi duniani wanatarajiwa kukutana nchini Qatar hii leo ili kufikiria uwezekano wa kupunguza uzalishaji wa bidhaa hiyo. Kuporomoka kwa bei ya mafuta kumeathiri uchumi wa nchi zenye utajiri wa mafuta  hususani  Nigeria, Venezuela na Urusi.  Maafisa kutoka mataifa hayo hivi sasa wanaandaa mpango utakaowezesha kupunguza uzalishaji wa mafuta  hali ambayo inaweza ikasababisha kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo.  Saudi Arabia ambayo ni nchi inayoongoza kuzalisha mafuta kwa wingi duniani  imesema itakubaliana na hatua ya kupunguza uzalishaji huo iwapo Iran nayo itakubali kufanya hivyo.  Hata hivyo  serikali ya Iran inaonekana kutokubaliana na mpango huo na inakusudia kususia kikao hicho  cha leo nchini Qatar. Hiyo ikiwa ni kwa mujibu wa shirika la habari la Iran- SHANA.

No comments:

Post a Comment