Monday, April 18, 2016


Watu zaidi  ya  270  wamekufa  kutokana  na  tetemeko la ardhi nchini Ecuador. Na wengine zaidi ya 2000  wamejeruhiwa. Tetemeko hilo lililofikia nguvu  ya 7.8  ya kipimo cha Richter liliikumba nchi hiyo  Jumamosi na kusababisha  madhara makubwa. Majengo mengi yalianguka na kuwafukia watu. Ingawa janga  hilo la asili lilichukua muda  wa  dakika  tano tu lilikuwa baya kabisa kuwahi kuikumba Ecuador katika muda  wa miaka 40 iliyopita. 
Wakati huo huo wafungwa  wapatao 100 walitoroka jela baada ya tetemeko hilo kutokea. Lakini  waziri  wa sheria  alifahamisha katika mtandao  wa  kijamii wa  twitter kwamba wafungwa 30  wamekamatwa tena katika  jimbo la Manabi magharibi  mwa  Ecuador.  

No comments:

Post a Comment