Saturday, April 16, 2016


Image result for Rais Rousseff
Rais wa Brazil Dilma Rousseff  hapo jana  ameendelea na jitihada za kupigania  kuendelea kubakia madarakani akifanya mikutano ya  faragha  muda mchache  kabla ya upigaji kura baadaye hii leo  utakaoamua iwapo kiongozi huyo atapelekwa katika bunge la Seneti ambako kesi dhidi yake inatarajiwa kufanyika.  Rousseff ambaye ni Rais wa kwanza mwanamke nchini humo  ameshutumu kile alichoita mipango  ya kutaka kumn'goa madarakani . Kiongozi huyo pia alifuta ratiba yake ya awali aliyopanga  kukutana na makundi ya waandamanaji wanaomuunga mkono na badala yake kujikita katika kutafuta kuungwa mkono na wabunge nchini humo.  Makamu wa Rais wa nchi hiyo Michel Temer ambaye sasa amegeuka kuwa hasimu wake na anayeongoza mapambano dhidi ya Rousseff   naye pia aliondoka mjini Sao Paulo kurejea mjini Brasilia   hatua ambayo vyombo vya habari nchini humo vimesema inaonyesha kuwepo  ushindani mkubwa katika suala hilo. Upinzani nchini Brazil unahitaji kiasi ya kura 342 kati ya kura 513   au theruthi mbili kutoka katika bunge la wawakilishi ili kuamua kumfikisha Rais Rousseff katika seneti ambako kesi  dhidi yake inaweza kufanyika.

No comments:

Post a Comment