Tuesday, March 8, 2016

Mwanafunzi aliyemtishia Trump kuondoka Marekani.


Elsayed
Mwanafunzi wa urubani kutoka Misri aliyeandika kwenye Facebook kwamba ulimwengu unaweza kumshukuru sana akimuua Donald Trump ameamua kuondoka Marekani kwa hiari.
Emadeldin Elsayed, 23, hakufunguliwa mashtaka yoyote ya uhalifu lakini maafisa wa Marekani walitaka afurushwe, wakili wake Hani Bushra amesema.
Maafisa wa hamiaji wamesema anaweza kuruhusiwa arejee nyumbani salama na kwa hiari mradi tu awe ameongoka kufikia tarehe 5 Julai.
Kwa sasa Elsayed anazuiliawa katika jela moja jimbo la California baada ya viza yake kufutiliwa mbali.
Bw Bushra alisema Jumatatu kwamba Elsayed anazuiliwa kinyume cha sheria.
“Anazuiliwa, nafikiri, kwa sababu yeye ni Mwislamu na mtu kutoka Mashariki ya Kati,” Bw Bushra aliambia shirika la habari la AP.
“Kijana huyu ataanza kutumiwa katika mabango ya kuichukia Marekani.”
Bw Elsayed alihojiwa na makachero wa Marekani mapema Februari baada yake kupakia picha ya Bw Trump kwenye Facebook na kuandika kwamba ako radhi kutumikia kifungo cha maisha jela kwa kumuua bilionea huyo na kwamba ulimwengu unaweza kumshukuru kwa hilo, Bw Bushra alisema.

No comments:

Post a Comment