Tuesday, June 7, 2016

UEFA Euro 2016
Ufaransa  itaimarisha  ulinzi katika  michezo ya kandanda ya  kombe  la  mataifa  ya  Ulaya, Euro 2016, ikiweka  zaidi ya  polisi  1,000 wa  ziada  na  wanajeshi.
Hatua  hizo  za  ziada zilitangazwa wakati  Ukraine imesema  imemkamata  Mfaransa  anayeshukiwa kupanga mashambulizi  kadhaa ya kigaidi wakati wa michezo  hiyo.
Kwa  jumla , zaidi  ya  polisi 90,000 , na  wanajeshi  pamoja na  wakala  wa  usalama watakuwapo kwa  muda  wote  wa mashindano  hayo  yatakayodumu  kwa  mwezi mzima  na yanaanza  rasmi  siku  ya  Ijumaa.
Naibu  meya  wa  jiji  la  Paris Jean Francois Martins amesema  kila  kitu kiko tayari  kwa  mashindano  hayo.
Kiasi ya mashabiki milioni 1.5 wanatarajiwa  kuhudhuria mashindano  hayo  yatakayokuwa  na  michezo 51 katika viwanja  10 nchini  Ufaransa.

No comments:

Post a Comment