Tuesday, May 31, 2016

Sudan yawafukuza raia 442 wa Eritrea.


Image copyrightAFP
Image captionOmar el Bashir
Serikali ya Sudan imewafurusha takriban raia 442 wa Eritrea ikiwemo wakimbizi sita waliosajiliwa kurudi nchini mwao mwezi huu kulingana na kundi moja la haki za kibinaadamu la Human Rights Watch.
''Sudan inawakamata na kuwalazimisha raia wa Eritrea kurudi katika serikali yao ilio na ukandamizaji bila kuwaruhusu wakimbizi kutafuta mahala pa kujilinda,alisema Gerry Simpson'',mkimbizi mwandamizi anayehusika na maswala ya utafiti katika HRW.
Sudan inafaa kufanya kazi na shirika la umoja wa mataifa kuhusu Ukimbizi ili kuwalinda,badala ya kuwarudisha nyumbani ili wakumbane na unyanyasaji,aliongezea.
Sudan haijatoa tamko lolote kuhusu madai hayo.

Mgogoro kuhusu sherehe ya siku ya uhuru Kenya.


Image captionViongozi wa Upinzani nchini Kenya
Mahakama kuu nchini Kenya inatarajiwa kutoa uamuzi wake iwapo muungano wa upinzani nchini Kenya CORD utaendelea na mkutano wao hapo kesho katika sherehe za Madaraka.
Hivi majuzi muungano huo wa upizani uliandamana ukishinikiza maafisa wakuu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (IEBC) kujiuzulu.
Maandamano hayo yalishuhudia vifo vya watu kadha na polisi kutumia nguvu kupita kiasi.
Muungano wa Cord umesema ulitaka kutumia siku hiyo kama siku ya kutafakari.
Image captionMaandamano ya Upinzani Kenya
Baraza la Taifa la Ushauri la Usalama limetoa tahadhari kwamba mikutano ya kisiasa katika jiji la Nairobi, linatishia usalama wa kitaifa.
Rais Uhuru Kenyatta anatarajiwa kuwahutubia watu siku hiyo ya madaraka mjini Nakuru magharibi mwa Kenya.

Wafanyakazi wataka Waziri aondolewe.


Image copyrightAP
Image captionWaziri Fabiano Silveira anayetuhumiwa kwa Rushwa
Wafanyakazi katika wizara inayopambana na rushwa nchini Brazil wameshindikiza kuondolewa kwa waziri wake mpya.
Maandamano hayo yanafuatiwa kutolewa kwa video ambayo Fabiano Silveira anatuhumiwa kusikika akikosoa uchunguzi wa rushwa katika kampuni ya mafuta ya serikali,Petrobras.Juma lililopita waziri wa mipango wa nchi hiyo alilazimishwa kuachia madaraka baada ya kukumbwa na shutuma kama hizo.Viongozi wote hao wawili walichaguliwa baada ya Rais Dilma Rousseff alipoondolewa madarakani.Amekuwa akisisitiza kwa muda mrefu kuwa mashitaka yaliyoundwa dhidi yake ni kwa ajili tu ya kuzuia upelelezi.

Monday, May 30, 2016

SLADS BAGAMOYO FULL VIDEO YA KILE KILICHOTOKEA KWENYE MAHAFALI NDOGO YA KUWAAGA WAHITIMU CHUONI HAPO.



siku ya ijumaa ya tarehe 27/05/2016 ilifanyika mahafali ndogo chuoni hapo ya kuwaaga wahitimu wa ngazi ya diploma ya certificate. na TING MUGOA nimekuwekea video ya kila kitu kilichofanyika chuoni hapo.

Dharuba na mvuwa kubwa zimesababisha mafuriko na watu watatu kufariki dunia katika jimbo la kusini magharibi mwa Ujerumani. Askari mmoja wa kikosi cha kukabiliana na maafa katika mji wa Schwäbisch Gmünd pamoja na mtu aliyekuwa akitaka kumuokoa ni miongoni mwa waliopoteza maisha, kwa mujibu wa taarifa ya wizara ya mambo ya ndani ya jimbo la Baden-Württemberg. Katika mji wa Weißbach karibu na Heilbronn mtu mmoja amekufa maji baada ya kuzama akiwa ndani ya gereji ya chini ya nyumba yake. Dharuba na mvuwa kubwa zimepelekea kima cha mito kupanda sana na haraka katika eneo hilo. Magari mengi yamefunikwa na maji na vikosi vya uokozi vimelazimika kuwaokoa watu kadhaa waliokwama ndani ya magari yao. Mvuwa kubwa na dharuba zimesababisha hasara kubwa pia katika mikoa ya Ansbach na Neustadt/Aisch katika jimbo la kusini la Bavaria.

Mpatanishi mkuu wa Syria ajiuzulu.


Image copyrightREUTERS
Image captionMpatanishi mkuu Syria
Mpatanishi mkuu wa muungano wa upinzani nchini Syria amejiuzulu katika kile anachosema kuwa, kuvunjika kwa mazungumzo ya amani, yenye nia ya kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu miaka mitano sasa.
Mohammad Alloush, anayetoka kwenye kamati kuu ya upatanishi HNC, amesema kuwa anajiondoa kwa sababu mazungumzo hayo yanayoungwa mkono na Umoja wa mataifa huko Geneva, hayajazaa matunda au kutanzua matatizo wanayopitia raia wa Syria waliozingirwa na vita.
Kamati kuu ya mazungumzo hayo ya amani iliahirisha shughuli zake mwezi Aprili na hakuna tarehe ambayo imewekwa ya kurejelewa kwa mazungumzo.

Walinda amani watano wauawa nchini Mali


Image captionWalinda amani wa Umoja wa Mataifa wanakabiliwa na changamoto ya usalama
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Mali umesema kuwa walinda amani wake watano wameuawa na wengine wamejeruhiwa vibaya katika shambulizi lililotokea katikati ya mji wa Mopti. Waathirika wanatokea nchini Togo.Gari lao lilipatwa na moto kabla ya kukanyaga bomu la ardhini,na kisha kulipuka.Waziri wa masuala ya kigeni nchini Mali, Abdoulaye Diop, ametuma salam za rambirambi katika mitandao ya kijamii kwa UN na nchi ya Togo.Vifo vyao vimekuja wakati dunia ikiadhimisha siku yawalinda amani.Mwaka uliopita walinda amani 129 kutoka umoja wa mataifa walipoteza maisha katika nchi 16 wanazofanyia shughuli zao.

Jeshi la Iraq laanza kukomboa mji wa falluja.


Image copyrightAFP
Image captionWanajeshi wa Iraq
Wanajeshi wa Iraq wameanza kile wanachokitaja kama mashambulio ya mwisho kabisa ya kuukomboa mji wa Fallujah, kutoka mikononi mwa wapiganaji wa Islamic State.
Fallujah ni mji ulioko kilomita 50 kutoka mji wa Baghdad, na umekuwa chini ya udhibiti wa IS kwa miaka miwili iliyopita.
Image copyrightAFPGETTY IMAGES
Image captionWanajeshi wa Iraq
Taarifa kutoka kwa idara ya usalama nchini Iraq, zinasema kuwa mapigano makali yamekuwa yakiendelea huko, tangu saa kumi na moja leo alfajiri.
Shambulio la hivi punde zaidi lilitekelezwa na kikosi maalum cha serikali cha kupambana na ugaidi, huku kikisaidiwa na majeshi ya muungano chini ya Marekani.
Image copyrightAFP
Image captionIslamic State
Yanashambulia Fallujah kutoka maeneo tatu tofauti, ili kuuzingira na kuziba kabisa njia za kukumbilia kwa wapiganaji hao wa IS.

Wanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma wafukuzwa.


Image captionChuo kikuu cha Dodoma
Wanafunzi katika chuo kikuu cha Dodoma nchini Tanzania wamefukuzwa chuoni humo baada ya kuzuka kwa mgogoro kati ya serikali na wahadhiri wa chuo hicho.
Wanafunzi hao waliagizwa kuondoka katika chuo hicho kufikia saa kumi na mbili jioni siku ya Jumapili.
Image captionIlani
Ilani hiyo imesema kuwa kulikuwa na makosa katika mafunzo ya wanafunzi wanaosomea shahada ya elimu ikiwemo sayansi,hesabati,teknolojia hivyobasi serikali imewataka wanfaunzi kuondoka chuoni humo hadi ilani yengine itakapotolewa.
Maelezo kuhusu mgogoro huo kati ya ya wahadhiri wa chuo hicho na serikali haujulikani.

Friday, May 27, 2016

MWENYEKITI WA BODI YA MAKTABA AWAASA WAHITIMU KUJIAJIRI.



leo ilikuwa ni mahafari ndogo ya kuwaaga wahitimu wa ngazi ya diploma na cheti chuoni SLADS, ambapo nafasi hiyo imetumika kuwaasa wahitimu kutotegemea ajira za mojakwa moja na hatimaye kutafuta nafasi nyingine za kujiajiri.







Ting Mugoa ninazi picha mbalimbali kutoka chuoni hapo.























     MWADILI WA CHUO.

MITUPIO
















Wednesday, May 25, 2016

Ushemeji wa Mhagama, Tanzanite One wamtia matatani Mbunge Millya.
May 25 2016 tayari nimezikusanya na waweza kuzipitia hapa chini moja baada ya nyingine, moja ya habari kubwa ni kutoka Gazeti la Jambo Leo  lenye kichwa cha habari ‘Ushemeji wa Mhagama, Tanzanite One wamtia matatani Mbunge Millya’.
Gazeti hilo limeeleza kuwa tuhuma za ushemeji kati ya Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenester Mhagama na mmoja wa wabia wa Kampuni ya Sky Associates inayomiliki Mgodi wa Tanzanite One zimelisukuma Bunge kumpa siku nne Mbunge wa Simanjiro ‘CHADEMA’ James Ole Millya athibitishe madai yake kwa ushahidi.
Gazeti hilo limeieleza nukuu ya maneno ya Millya alipokuwa akitoa madai hayo alipokuwa akichangia mjadala bungeni iliyonukuliwa na Naibu Spika, Dk. Tulia ….>>> ‘Sheria za kazi zinajulikana, ni bahati mbaya kwamba Mhagama anatajwa kwamba ni shemeji wa mmoja wa wabia wa hapo. Dada anaitwa Asia Gonga ameolewa na Martin au Yusuph Mhagama’

 Tuhuma za Ushemeji wa Waziri Mhagama, Tanzanite One zimelisukuma bunge kumpa siku 4 Millya athibitishe
BAADA YA JACKLINE WOLPER KUWA NA HARMONIZE, KATAJA JINA ANALOMUITA DIAMOND KWA SASA. 

Image result for jackline wolper
Kwa sasa headlines nyingi katika upande wa mastaa Tanzania ni stori kuhusu penzi la muigizaji Jackline Wolper na msanii wa Bongo fleva kutoka Wasafi Classic Baby (WCB)Harmonize ndio Topic kubwa town.
Katika mahojiano na Take One ya Clouds TV  na Zamaradi MketemaJackline Wolperameeleza mambo kadhaa kuhusiana na penzi lake la HarmonizeDiamond ambaye aliwahi kuwa mpenzi wake anachukuliaje mahusiano yao?
“Diamond rafiki yangu sana ni mtu ambae nategemea hata kuja kufanya nae filamu, Diamondi ni rafiki yangu sana licha ya watu wanaweza wasielewe, lakini sasa hivi Diamond ni baba mkwe wangu,
“kuhusu Harmonize nampenda kwa sababu ana hofu ya mungu, ana heshima sana mwisho hawezi kufanya maamuzi bila kuomba ushauri, katika kunipenda mimi alipiatia pia kuomba ushauri kwa Diamond ambaye ni boss wake kaka yake na kupewa ruhusa kwa hiyo Baraka zimetoka kwa Diamond mwenyewe”

Bill Cosby atakiwa mahakani


Image copyrightREUTERS
Jaji nchini Marekani ameamuaru mchekeshaji, Bill Cosby, kusimama mahakamani dhidi ya kesi kwa madai ya unyanyasaji wa kijinsia.
Cosby anatuhumiwa kwa makosa ya kumdhalilisha wanawake katika makazi yake mnamo mwaka 2004 baada ya kumlewesha kwa kitu kinachodaiwa dawa za kulevya.
Mchekeshaji huyo,ambaye awali kabla ya masahibu haya alikuwa ni mmoja miongoni mwa wachekeshaji maarufu wa runinga nchini Marekani, tayari amekwisha kumbana na misukosuko ya kukabiliwa na wimbi la madai unyanyasaji wa kijinsia.
Wanawake waliowengi, ambao alikuwa na mahusiano nao miaka ya 1960 wao hawawezi tena kufungua mashtaka ya jinai.Kufuatia hali hiyo Cosby amekana madai yote yanayomkabili.
Mwezi uliopita mahakama ya rufaa ilitupilia mbali madai yanayomkabili Cosby na kusema kwamba alikuwa kinga ya mashtaka kutoka upande wa mashitaka na aliyekuwa Mwanasheria wa wilaya muongo mmoja uliopita.