Friday, May 6, 2016

Image result for LIVERPOOL
Klabu  ya  Liverpool  ya  Uingereza  itapambana  na  Servilla  ya Uhispania  katika  fainali  ya  ligi  ya  Ulaya , Europa League, itakayofanyika  katika  mji  wa  Basel  nchini  Uswisi mwezi  huu.
Klabu  hiyo  ya  Uingereza  ilizidi  ngumu  timu  hiyo  ya  Uhispania jana  usiku nyumbani, na  kuishinda  kwa  mabao 3-0 katika mkondo  wa  pili  wa  nusu  fainali  na  kushinda  kwa  jumla  ya mabao  3-1 baada  ya  michezo  miwili.
Katika  nusu  fainali  nyingine , Sevilla iliishinda  Shaktar Donetsk kwa  mabao 3-1 nyumbani  na  kusonga mbele  kwa  jumla  ya mabao 5-3.
Timu  hizo  mbili zitapambana  katika  fainali mjini  Basel Mei 18, ambapo  mshindi  moja  kwa  moja  anapata  nafasi  ya  kucheza katika  Champions League.
Sevilla, ikiwa  ya  saba  katika  msimamo  wa  ligi  ya  Uhispania, italenga  kupata  taji  la  tatu  mfululizo  la  Ligi  ya  Ulaya.

No comments:

Post a Comment