Friday, May 6, 2016

Image result for Waziri mkuu Uturuki
Waziri  mkuu  wa  Uturuki Ahmet Davutoglu  ametangaza  kuwa atajiuzulu  katika  muda  wa  wiki  mbili  zijazo  wadhifa  wa mkuu  wa  chama  tawala  na  waziri  mkuu.
Uhusiano  kati  ya  waziri  huyo  mkuu  na  rais Recep Tayyip Erdogan , umedhoofika  katika  wiki  za  hivi  karibuni.
Uamuzi  wa  waziri  mkuu  huyo  kujiuzulu unakuja  katika  wakati wa matatizo  nchini  Uturuki , ikiwa  ni  pamoja  na kampeni  ya kijeshi dhidi  ya  watu  wanaotaka  kujitenga, ugaidi, rushwa  na ukandamizaji  wa  vyombo vya binafsi  vya  habari.
Josh Earnest , msemaji  wa  Ikulu  ya  Marekani , White House, amesema  mabadiliko  hayo  hayataathiri ushirikiano  kati  ya nchi  hizo  mbili  katika  mapambano  yao dhidi  ya  kile kinachojulikana  kama  kundi  la  kigaidi  la  Dola  la  Kiislamu, linalojulikana  kama  IS.
Chama  tawala  cha  Haki  na  Maendeleo kitafanya  mkutano wake  maalum  baadaye  mwezi  huu  kumchagua  mrithi  wa Davutoglu.

No comments:

Post a Comment