Thursday, January 7, 2016

Irain yasema Saudi Arabia imeshambulia ubalozi


IranImage copyrightnone
Image captionIran huongozwa na Washia nayo Saudi Arabia huongozwa na Wasuni
Iran imesema Saudi Arabia imeshambulia ubalozi wake nchini Yemen kwa makombora.
Kituo cha utangazaji cha Iran cha Irinn kimesema makombora yalianguka katika majengo ya ubalozi huo na kusababisha uharibifu.
Wakazi wa Sanaa wanasema kulitokea mashambulio kadha kutoka angani asubuhi, yakitekelezwa na majeshi ya muungano unaoongozwa na Saudi Arabia dhidi ya waasi wa Houthi.
Uhusiano kati ya nchi hizo mbili umedorora tangu kuuawa kwa mhubiri wa Kishia Sheikh Nimr al-Nimr aliyeshtakiwa makosa yanayohusiana na ugaidi nchini Saudi Arabia.
Ubalozi wa Saudi Arabia mjini Tehran ulishambuliwa na kuchomwa moto na waandamanaji wakati wa maandamano yaliyotokea maeneo ya Washia kulalamikia mauaji hayo.
Saudi Arabia nayo ilijibu kwa kukatiza uhusiano wa kidiplomasia na Iran, hatua ambayo washirika wake kama vile Bahrain, UAE, Kuwati, Sudan, Somalia na Djibouti walifuata.
Iran na Saudi Arabia zimekuwa zikiunga mkono makundi pinzani katika mizozo inayoendelea nchini Syria na Yemen.

No comments:

Post a Comment