Friday, January 15, 2016


Image result for Rais Buhari
Rais wa Nigeria Mohammadu Buhari ameahidi  kuanzisha uchunguzi mpya  kuhusiana na tukio la kutekwa nyara  wasichana zaidi ya 200 wa shule  ya Chibok katika  jimbo la Borno nchini humo  na kundi la itikadi kali la  Boko Haram.   Kauli hiyo ya Rais Buhari inafuatia maandamano yaliyoongozwa  na wazazi wapatao 300 na makundi mengine ya wanaharakati  katika mji wa Abuja wakiwa wamebeba mabango ya picha zinazoonyesha sura za  baadhi ya wasichana hao waliotekwa kabla ya waandamanaji hao  kubebwa katika mabasi na kupelekwa kwenda kukutana kwa mazungumzo na Rais Buhari katika makazi yake. Hii ni mara ya kwanza kwa makundi ya waandamanaji hao na makundi mengine yanayoongoza harakati za kushinikiza kurejeshwa kwa wasichana hao wakiwa hai kukutana na Rais Buhari tangu alipotangaza mwezi Desemba ya kuwa kundi hilo la itikadi kali linaonekana kushindwa kimbinu  licha ya wachambuzi wa masuala ya kiusalama kuonya  kuwa mapambano dhidi ya kundi hilo bado yanahitajika kwa kiwango kikubwa. Rais Buhari aliwaambia waandamanji hao kuwa  mshauri wa taifa hilo  wa masuala ya kiusalama Babagana Monguno ataunda kamati maalumu kwa ajili ya kuanzisha uchunguzi mpya kuhusiana na kutekwa  kwa wasichana hao.

No comments:

Post a Comment