Sunday, January 10, 2016


Mahakama ya katiba nchini Niger jana imeidhinisha wagombea 15 wa urais katika uchaguzi utakaofanyika mwezi ujao. Miongoni mwao ni kiongozi wa kisiasa na mpinzani Hama Amadou, ambaye alifungwa miezi miwili iliyopita baada ya kurudi uhamishoni alikokuwa kwa zaidi ya mwaka mzima. Kuna uwezekano wa mahakama ya katiba kukishinikiza chama tawala kumuachia huru Amadou, ambaye anatarajiwa kuwa miongoni mwa wagombea watatu watakaoongoza katika uchaguzi huo wa Februari 21. Maafisa nchini Niger walimkamata Amadou mwezi Novemba, katika uchunguzi uliohusisha genge linalotuhumiwa  kuwachukua  watoto  wachanga  kutoka  kile kinachoelezwa  kama "viwanda vya  kuzalisha watoto" katika nchi jirani ya Nigeria.

No comments:

Post a Comment