Friday, January 29, 2016


Wanaharakati watatu wa haki za binaadamu nchini China wamehukumiwa kifungo jela. Kwa mujibu wa shirika linalopigania haki za binaadamu Amnesty International,wakili,mpigania haki za binaadamu Tang Jingling amehukumiwa kifungo cha miaka mitano jela. Washitakiwa wenzake pia wamehukumiwa kifungo jela, Yuan Xinting amehukumiwa miaka mitatu, na Wang Qingying miaka miwili na nusu. Katika kesi yao iliyosikilizwa katika mji wa Kanton,watuhumiwa hao watatu walishitakiwa kwa makosa ya kusambaza vitabu vinavyozungumzia mapambano bila ya matumizi ya nguvu.Tangu alipoingia madarakani rais Xi Jinping miaka mitatu iliyopita,wapinzani kadhaa wamehukumiwa kutumikia kifungo jela nchini China.

No comments:

Post a Comment