Friday, January 29, 2016

\
Image result for obama
 Rais Barack Obama wa Marekani amehimiza juhudi kubwa zaidi zichukuliwe kuwazuwia wanamgambo wa dola la kiislam wasienee nchini Libya. Kwa mujibu wa Ikulu ya Marekani,rais Obama amemtaka mshauri wake wa masuala ya usalama azidishe makali ya mapambano dhidi ya magaidi nchini Libya na katika nchi nyenginezo. Kabla ya hapo waziri wa ulinzi Ashton Carter alisema wanamgambo wa IS wanajenga kambi za mazoezi nchini Libya na kuwaandikisha pia wapiganaji wa kigeni. Ili kuzuwia kuenea kitisho cha itikadi kali kama kile cha Irak na Syria,Marekani inazingatia mikakati tofauti. Jumatano iliyopita, mwakilishi mmoja wa wizara ya ulinzi ya Marekani-Pentagon alizungumzia kuhusu kuchunguzwa uwezekano wa kuanzishwa opereshini za kijeshi nchini Libya.

No comments:

Post a Comment