Thursday, January 7, 2016

Waliokuwa wakila nyasi na udongo Syria kusaidiwa


Image copyrightAP
Image captionBashar Al Assad
Umoja wa Mataifa umesema serikali ya Syria imekubali kuruhusu misaada ya kibinadamu kwenda katika mji ulizingirwa wa Madaya ambayo kuna taarifa watu wamekuwa wakifa kwa njaa.
Shirika la Chakula la Umoja wa Mataifa limeiambia BBC kuwa msafara wa umeingia katika mji ulikuwa ukikaliwa na waasi katibu na mpaka na Lebanon.
Madaya ulilkuwa umezingirwa na majeshi ya serikali na wafuasi wao wa Hezbollah kwa miezi kadhaa picha za video katika eneo hilo zinaonyesha watu wakiwa katika hali mbaya. Inaelezwa kuwa baadhi yao wamekuwa wakilazimika kula majani na udogo badaa ya chakula kumalizika.
Mkuu wa shirika la chakala duniani katika ofisi za London Grey Barrow amesema maandalizi yanafanyika kuhakikisha misaada inawafikia wanaohitaji.
"Kumekuwa na mipango inayofanyika kabla ya magari kuingia eneo hilo labda inaweza kuwa ndani ya saa sabini na mbili labda hilo ndilo linaweza kuwezekana. Ninaamami hadi jumatatu tutapeleka magarai eneo hilo magari ambayo yapo tayari lakini yanahitaji mipango."
Hata hivyo Grey ametahadharisha eneo wanalopeleka misaada ni eneo la hatari.
"Nadhani ni lazima tukubali tunakoenda hali ni mbaya. Tunakwenda eneo la mstari wa mbele tunapaswa kujua tunapoingia pale hakuna hatari ya kudhurika, kwamba tutapeleka chakula huko na mahitaji mengine tutakayobeba kwa niaba ya mashirika mengine ya kibinadamu na tunadhani tutawafikia wale wenye mahitaji makubwa."

No comments:

Post a Comment