Wednesday, January 6, 2016

Wananchi wa Jamhuri ya Afrika Kati wanasubiri kwa hamu matokeo ya uchaguzi unaozusha mabishano. Kwa mujibu wa matokeo ya awali mawaziri wakuu wawili wa zamani wanaonyesha kujikingia kura zinazolingana. Serikali ya Jamhuri ya Afrika kati ilipinga fikra ya kusitisha zoezi la uchaguzi baada wagombea karibu 20 kudai zoezi hilo lizuwiliwe wakihoji duru ya kwanza iligubikwa na visa vya udanganyifu. Duru ya pili ya uchaguzi imepangwa kuitishwa Januari 31 ijayo.

No comments:

Post a Comment