Friday, February 26, 2016


Image result for syria
Image result for al shabaab
Kiasi ya watu  zaidi ya tisa wakiwemo raia  wameripotiwa kuuawa nchini Somalia katika tukio lililohusisha mashambulizi ya risasi kati ya watu wanaodaiwa kuwa wanamgambo wa kundi la itikadi kali la Al- Shabab na walinzi wa hoteli moja iliyoko katika mji mkuu wa nchi hiyo , Mogadishu kabla ya vikosi vya usalama vya serikali kuingilia kati na kuzima shambulio hilo. Duru kutoka nchini humo zinaarifu kuwa kiasi ya wanamgambo watano waliuawa  huku pia raia tisa wakidaiwa kuuawa katika tukio hilo. Mtu mmoja aliyekuwa amebeba miripuko katika gari  alijiripua kwa kujitoa muhanga baada ya kuliingiza gari hilo kwa nguvu katika lango la hoteli hiyo ijulikanayo kama SYL hapo jana usiku na kutoa mwanya kwa  watu waliokuwa na bunduki kutumia fursa hiyo kujaribu kulazimisha kupita katika kizuizi cha kwanza cha ulinzi ingawa washambuliaji hao hawakufanikiwa kupita katika kizuizi cha pili cha lango la hoteli hiyo. Washambuliaji wanne waliokuwa na bunduki pamoja na mtu aliyejitoa muhanga ni miongoni mwa waliouawa katika tukio hilo.  Kundi la Al- Shababu limedai kuhusika na shambulizi hilo.

Mwigizaji wa filamu ya Rocky Tony Burton afariki.


Image captionMarehemu Tony Burton kushoto na Sylvester Stalone
Tony Burton aliyeshiriki katika filamu sita za Rocky dhidi ya Sylvester Stallone amefariki akiwa na umri wa miaka 78.
Kiini cha kifo chake bado hakijulikani ,lakini dadaake ,Loretta Kelly amesema kuwa amekuwa akienda hospitalini katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.
Ameongozea kuwa hajapata utambuzi wa ugonjwa wake katika wakati huo na kwamba hali yake ya afya ilikuwa imezorota hali ya kutoweza kuiona filamu ya Creed.
Uigizaji wake ulimsaidia Creed ambaye ni mpinzani wa Rocky Balboa katika filamu mbili za kwanza za masumbwi kabla ya kuwa mkufunzi wa Balboa.
TCU YAHAMIA ARUSHA NA SAKATA LA KUVIFUTIA VIBALI VYUO VISIVYO KIDHI.
Image result for mt.Yosefu university
February 26 2016 taarifa kutoka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU)ilikuwa ni hii ya kukifutia kibali Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania (SJUIT), kampasi ya Arusha na kuwahamisha wanafunzi wote waliokuwa wanasoma katika kampasi hiyo kwa gharama za Chuo hicho.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini Prof. Yunus Mgaya amesema ‘Kwa muda mrefu na kwa wakati tofauti kumekuwapo na matukio ya migogoro baina ya uongozi wa Chuo na Wanafunzi, Kwa kipindi hicho chote tumekuwa tukifuatilia kwa ukaribu chimbuko la migogoro hiyo na kuchukua hatua stahiki

Gianni Infantino ndio rais mpya wa Fifa.


Image result for Gianni Infantino



Image copyright

Raia wa Switzerland Gianni Infantino amechukua mahala pake Sepp Blatter kama rais wa shirikisho la soka duniani Fifa.
katibu huyo mkuu wa Fifa alipata kura 115 katika raundi ya pili ikiwa ni kura 27 zaidi ya mpinzani wake wa karibu Sheikh Salman bin Ebrahim al-Khalifa.
Mwanamfalme Ali bin al-Hussein alikuwa wa tatu akiwa na kura nne huku Jerome Champagne akishindwa kupata hata kura moja.
Tokyo Sexwale alijiondoa kabla ya kura kuanza kupigwa mjini Zurich.

Raundi ya kwanza ya upigaji kura ilishindwa kum'baini mshindi wa moja kwa moja.
Wingi wowote wa kura[zaidi ya aslimia 50] katika raundi ya pili ya uchaguzi huo ulikuwa unaweza kumwezesha mgombea kutangazwa mshindi katika raundi ya pili.
Infantino ni wakili mwenye umri wa miaka 45 kutoka eneo la Brig jimbo la Valais nchini Switzerland ,ikiwa ni eneo lililopo chini ya maili sita kutoka nyumbani kwa Blatter.
Blatter ambaye aliliongoza shirikisho hilo tangu mwaka 1998 alijiondoa mwaka uliopita kabla ya kupigwa marufuku katika shughuli zozote za kandanda kwa kipindi cha miaka sita .

Baada ya kutangazwa mshindi, Infantino aliwaambia wajumbe waliopiga kura kwamba hakuweza kujielezea kutokana na hisia alizokuwa nazo.
Lakini aliwaambia wajumbe kwamba ''kwa pamoja wataweza kuirudisha sura ya Fifa na heshima ya Fifa''.

Wednesday, February 24, 2016

Uchumi wa Afrika Kusini uko 'taabani'


Image copyrightReuters
Image captionWaziri wa Fedha Pravin Gordhan
Uchumi wa taifa la Afrika Kusini uko katika hali mbaya,waziri wa fedha nchini humo Pravin Gordhan amesema.
Tamko hilo lilijiri kabla ya hotuba yake ya matumizi ya serikali ambapo alipunguza takwimu za ukuwaji wa uchumi wa taifa hilo kutoka asilimia 1.7 hadi 0.9.
Alikiri kwamba uchumi unazorota kutokana na kupungua kwa ukuaji wake, asilimia 25 ya ukosefu wa ajira na kuenea kwa umasikini.
Sarufi ya Afrika kusini Rand ambayo imeshuka katika kipindi cha miaka mitano ilianguka tena wakati alipokuwa akitoa hotuba hiyo.
Image captionSarufi ya Afrika kusini Rand
Bwana Gordhan alitangaza kuongezeka kwa viwango vya kodi ya ushuru, faida ya mtaji, mafuta, vinywaji vyenye sukari, pombe na tumbaku pamoja na ushuru wa mazingira ambao unatarajiwa kuleta randi bilioni 18 sawa na dola bilioni 1.18.
Alikuwa ametarajiwa kutangaza mipango ya kubinafsisha mali ya serikali,lakini alisema kuwa mipango inaendelea ya kuunganisha shirika la ndege la taifa hilo lenye hasara na shirika la ndege linalomilikiwa na serikali la SA Express.

Image result for RAIS Morales
Rais  wa  Bolivia  Evo  Morales ameshindwa  katika  juhudi zake  za  kutaka muhula  wa  nne  madarakani, ikiwa  ni kushindwa  kwake kwa  mara  ya  kwanza  katika  uchaguzi tangu  kuingia  madarakani mwaka  2006.
Morales  mwenye  umri  wa  miaka  56, amekuwa madarakani  kwa  muongo  mmoja, akiungwa  mkono  zaidi na  makundi  ya  wazalendo pamoja  na  matawi  ya  vijijini katika  nchi  hiyo  masikini  zaidi  katika  bara  la  Amerika.
Wakati  akikataa  kukubali  matokeo  hadi  mwisho, Morales ameahidi  kuheshimu  matokeo  rasmi  baada  ya  uchaguzi wa  hapo  Jumapili  kuhusiana  na  mabadiliko  katika katiba  ambayo  yangemruhusu  kugombea  tena  na kurefusha utawala  wake  hadi  miaka  19.  Kipindi  chake cha  sasa  cha  utawala  kinamalizika  mwaka  2020.
Wakati  asilimia  99.72  za kura  zimekwisha  hesabiwa , rais  wa  tume  ya  uchaguzi  Katia Uriona  amesema kwamba  asilimia  51.3  ya  wapiga  kura  wamesema hapana  katika  kura  hiyo  ya  maoni, dhidi  ya  asilimia 48.7  ambao  wamesema  ndio.