Wednesday, February 3, 2016


Image result for ugaidi
Iran  na  Ujerumani  zimekubaliana  kuhusu  haja  ya  kuwa na  ushirikiano  kupambana  na  ugaidi. Hayo yamebainika leo  wakati  waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Ujerumani Frank-Walter Steinmeier  akiwa  afisa  wa  ngazi  ya  juu wa  hivi  karibuni  kufanya  ziara  nchini  Iran tangu  kuanza kutekelezwa kwa makubaliano  ya  kihistoria  ya  nyuklia.
Rais  wa  Iran  Hassan Rouhani  amesema  nchi  hizo  mbili zinaweza  kushirikiana  katika  kutatua  mizozo  ya  kikanda na  kimataifa, hususan  katika  kupambana  na  ugaidi. Rouhani  amesema  hali  ya  upatikanaji  wa silaha  na fedha  kwa ajili  ya  ugaidi  ni  lazima  ikomeshwe.
Ziara  ya  Steimeier  imekuja  baada  ya  makubaliano  ya kihistoria  kati  ya  Iran  na  mataifa  yenye  nguvu  duniani kuweka  ukomo katika  mpango  wa  kinyuklia  wa  Iran  ili kuweza  kuondolewa  vikwazo  vya  kimataifa.
Waziri  Steinmeier atakwenda  Saudi  Arabia  baada  ya ziara  hiyo  nchini  Iran.

No comments:

Post a Comment