Wednesday, February 24, 2016


Image result for RAIS Morales
Rais  wa  Bolivia  Evo  Morales ameshindwa  katika  juhudi zake  za  kutaka muhula  wa  nne  madarakani, ikiwa  ni kushindwa  kwake kwa  mara  ya  kwanza  katika  uchaguzi tangu  kuingia  madarakani mwaka  2006.
Morales  mwenye  umri  wa  miaka  56, amekuwa madarakani  kwa  muongo  mmoja, akiungwa  mkono  zaidi na  makundi  ya  wazalendo pamoja  na  matawi  ya  vijijini katika  nchi  hiyo  masikini  zaidi  katika  bara  la  Amerika.
Wakati  akikataa  kukubali  matokeo  hadi  mwisho, Morales ameahidi  kuheshimu  matokeo  rasmi  baada  ya  uchaguzi wa  hapo  Jumapili  kuhusiana  na  mabadiliko  katika katiba  ambayo  yangemruhusu  kugombea  tena  na kurefusha utawala  wake  hadi  miaka  19.  Kipindi  chake cha  sasa  cha  utawala  kinamalizika  mwaka  2020.
Wakati  asilimia  99.72  za kura  zimekwisha  hesabiwa , rais  wa  tume  ya  uchaguzi  Katia Uriona  amesema kwamba  asilimia  51.3  ya  wapiga  kura  wamesema hapana  katika  kura  hiyo  ya  maoni, dhidi  ya  asilimia 48.7  ambao  wamesema  ndio.

No comments:

Post a Comment