Thursday, February 11, 2016


Image result for UN
Umoja  wa  Mataifa  unataka  kutuma  wataalamu huru  wa wanaoweza  kutambua alama za  eneo la tukio  nchini Burundi  kuwasaidia  maafisa  wanaochunguza  kuhusu makaburi  yaliyozikwa  watu  wengi  katika  nchi  hiyo iliyokumbwa  na  mzozo.
Baada  ya ukandamizaji  wa  majeshi  ya  usalama  nchini Burundi  mwezi  Desemba  dhidi  ya  waandamanaji , watu walioshuhudia  wamejitokeza  na  kutoa  maelezo  ya kuwapo  kwa  kiasi  ya  makaburi  tisa  yaliyozikwa  watu wengi  ndani  na  nje  ya  mji  mkuu  Bujumbura  ikiwa  ni pamoja  na  moja  katika  kambi  ya  jeshi.
Burundi  imekuwa  katika  hali  ya  ghasia  tangu  rais Pierre  Nkurunziza  kutangaza  mipango mwezi  Aprili mwaka  jana  ya  kuwania  muhula  wa  tatu  madarakani. Zaidi  ya  watu  400 wameuwawa  katika  ghasia  na  kiasi ya  wengine  230,000  wameikimbia  nchi  hiyo.
Jana  Jumatano Marekani  iliishutumu  Rwanda  kwa kuhusika  na  vitendo  vya  kuidhoofisha  nchi  hiyo, ikiwa ni  pamoja  na  kuwaorodhesha  wakimbizi  kwa  nia  ya kuishambulia serikali  ya  Burundi.

No comments:

Post a Comment