Thursday, November 26, 2015

Adam Juma kayaandika haya kwa madirector wenzake……


Muongozaji wa video za Bongo Adam Juma leo ameandika ujumbe ambao inawezekana ukawahusu baadhi ya waongozaji wengine wa video za Tanzania.
Kwa madirector wadogo na wakubwa, hakuna mafanikio yanakuja kirahisi rahisi, hakuna media itakayokuokoa katika ukame wa kazi utakapo wasili. Sifa hujenga kiburi akili hujenga ustaarabu, mafanikio yako yapo mkononi mwako- hata wakishoot mbinguni isiwe sababu ya wewe kuacha na kutoipenda kazi yako‘ – Adam Juma
Simama kwenye mstari na ujiamini, usishindane na upepo wa dunia hautashinda. Hakuna anayeweza akawa namba 1 kila siku na ukilijua hili utalala vizuri bila mawazo. Kila kazi ya mikono yangu ni zawadi kwa atakayeipenda na kuichukia, najiamini na naipenda kazi yangu. Ubunifu ndio utakao tuokoa katika ukame huu na sio budget, uongo, chuki na majigambo. Stay blessed all’Adam Juma

No comments:

Post a Comment