Monday, November 30, 2015

Wachimba mgodi 5 wafariki Geita Tanzania

 
Wachimbaji dhahabu watano wamefariki baada ya kufukiwa na kifusi huko Geita
Wachimbaji dhahabu watano wamefariki baada ya kufukiwa na kifusi katika machimbo ya Mgusu mkoani Geita, Kusini Kaskazini mwa Tanzania.
Mwandishi wa BBC Sammy Awami anaarifu kuwa ,tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Jumapili katika machimbo yanayomilikiwa na kampuni ya Geita Gold Mine ambayo ni moja ya makampuni makubwa ya uchambaji wa dhahabu barani Afrika.
Makamu wa rais wa kampuni hiyo Simon Shayo ameiambia BBC kwamba miili hiyo iliokolewa jana kwa ushirikiano na wachimbaji wengine wa eneo hilo.
Shayo alisema eneo ambalo tukio hilo lilitokea si eneo salama na kwamba lilipigwa marufuku kwa shughuli za uchimbaji.
Hata hivyo baadhi ya wachimbaji wamekuwa wakiendelea kuingia na kufanya shughuli za uchimbaji kinyemela na kupuuza ilani ya kutoingia katika maeneo hayo.
 
Wiki mbili tu zilizopita, wachimbaji wengine watano waliokolewa wakiwa hai katika machimbo ya Nyangalata baada ya kufukiwa na kifusi kwa siku 41.
Wiki mbili tu zilizopita, wachimbaji wengine watano waliokolewa wakiwa hai katika machimbo ya Nyangalata baada ya kufukiwa na kifusi kwa siku 41.
Wanne wao bado wako hospitalini, wakati mmoja alifariki dunia wiki iliyopita.

No comments:

Post a Comment