Wednesday, November 25, 2015

Gambia yapiga marufuku tohara ya wanawake

Gambia yapiga marufuku tohara ya wanawake
Rais wa Gambia, Yahya Jammeh,amepiga marufuku tohara ya wanawake nchini humo akisema inakwenda kinyume na mafundisho ya kiislamu.
Umoja wa mataifa unasema karibu robo tatu za wanawake wa Gambia wamefanyiwa ukeketaji.
Watabibu wamekuwa wakieleza matatizo ya kiafya yanayotokea kutokana na tabia hiyo lakini hilo halijapunguza visa vya upashaji tohara wanawake nchini hiumo.
 
Madaktari wamekuwa wakielezea matatizo ya kiafya yanayotokana na kupashwa tohara kwa wanawake
Sasa rais Yahya Jameh amesema amekuwa akitafiti kwa muda wa miaka 21 katika kitabu tukufu cha Quran na vilevile kupitia mahojiano na wanazuoni wa kiislamu na hamna ushahidi wowote wa kufungamanisha kitendo hicho na dini ya Kiislamu.

No comments:

Post a Comment