Monday, November 30, 2015

Kipigo cha Ethiopia chawarejesha Kilimanjaro Stars Tanzania, Full Time ya CECAFA Nov 30

Michuano ya mataifa ya Afrika Mashariki na Kati maarufu kama CECAFA Senior Challenge Cup yameendelea leo November 30 kwa kupigwa mechi za kwanza za robo fainali ya michuano hiyo, miongoni mwa mechi za robo fainali zilizochezwa leo November 30 ni mechi kati ya timu ya taifa ya Tanzania bara maarufu kama Kilimanjaro Stars ilicheza dhidi ya mwenyeji wa mashindano hayo timu ya taifa ya Ethiopia.
EthiopiaStars
Hii ni mechi ya robo fainali iliyokuwa inazikutanisha timu zilizokuwa kundi moja na mchezo wao wa mwisho walicheza na kumaliza kwa sare ya goli 1-1, November 30 Kilimanjaro Stars ilicheza mchezo huo ikiwa na kikosi chake kamili lakini kilikuwa na mabadiliko kidogo. Mchezo huo ambao Kilimanjaro Stars walianza kwa kupata goli la kuongoza kupitia kwa nahodha wao John Bocco dakika ya 24, dakika 90 zilimalizika kwa sare ya goli 1-1 baada ya Panom Cathuoch kuisawazishia goli Ethiopia dakika 57.
Ethiopia-cecafa
Kwa kawaida ya michuano hiyo kwa mechi za robo fainali umaliziwa kwa mikwaju ya penati kama dakika 90 zitamalizika kwa sare yaani bila kupata mshindi, hapo ndipo Kilimanjaro Stars ilikosa bahati na Ethiopia kufuzu hatua inayofuata kwa kwa kufanikiwa kushinda jumla ya penati 4-3.

No comments:

Post a Comment