Monday, November 30, 2015

EU, Uturuki zakubaliana suala wakimbizi

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan
Umoja wa ulaya na uturuki wafikia makubaliano ya jinsi ya kuchukua hatua ili kuondokana na mafuriko ya wakimbizi na wahamiaji ndani ya bara la Ulaya, mkutano huo umefanyika nchini Ubeljiji katika makao maku ya EU.
Chini ya makubaliano hayodolla bilioni 3 zitatolewa na Umoja huo(EU) ili kusaidia wakimbizi kutoka nchi ya Syria wanaoelekea Uturuki.
Tayari Ankara imeshatumia dolla billioni 8 kutatua matatizo mbali mbali ya wageni hao.
Mazungumzo hayo yali fufua pia mjadala ju ya Uturuki kujiunga katika nchi zenye kuunda Umoja wa Ulaya na likazungumzwa pia la nchi hiyo kusafiri bila mipaka ndani ya bara hilo katika maeneo yaliyokubaliwa kutumia visa moja iitwayo shcenghen.
Waziri mku wa Uturuki Ahmet Davutoglu amesema ni tukio la kihistoria katika mahusiano ya ututruki na Umoja wa Ulaya.

No comments:

Post a Comment