Thursday, November 26, 2015

Urusi kushirikiana kupambana na IS

 
 Rais wa Urusi Vladmir Putin na mwenziye wa Ufaransa Francois Hollande
Urusi imesema iko tayari kushirikiana katika mapambano dhidi ya kundi la kigaidi la Islamic State.
Rais Vladmir Putin amemwambia mweziye wa Ufaransa Francois Hollande, kuwa shambulio dhidi ya ndege ya abiria ya Urusi na lile lililotokea mjini Paris, ambayo yote kundi la Islamic State limekiri kuhusika, kumefanya nchi hizo kuungana dhidi ya adui wao huyo.
Rais huyo wa Ufaransa yupo nchini Urusi kama sehemu ya kujaribu kutafuta muungano kuweza kuwadhibiti wapiganaji wa Islamic state nchini Syria.

No comments:

Post a Comment