Friday, November 13, 2015

ICC yapunguza kifungo cha Katanga

 Katanga alikuwa wa pili kuhukumiwa na mahakama ya ICC
Majaji wa rufaa katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC wamepunguza hukumu aliyopewa kiongozi wa zamani wa waasi nchini Congo Germain Katanga.
ICC imesema kifungo cha Katanga kilichokuwa miaka 12 kitapunguzwa kwa miaka mitatu na miezi minane.
Majaji wamefanya uamuzi huo kwa kuwa alisema anajutia matendo aliyoyatenda, anajitenga na uhalifu uliofanywa na wanaona kwamba anaweza akatafutiwa pahali pa kukaa.
Katanga alipatikana na makosa ya kupanga shambulio katika vijiji na kwa mauaji ya raia wengi vijiji vilivyo kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo mwaka 2003.
Sasa ataachiliwa huru Januari 18, 2016.

No comments:

Post a Comment