IS lajipatia zaidi ya $500m kupitia mafuta
Islamic State
Kundi la wapiganaji
wa Islamic State limejipatia zaidi ya dola milioni 500 kupitia uuzaji
wa mafuta kulingana na afisa mmoja wa wizara ya fedha nchini Marekani.
Mteja wake mkubwa amekuwa rais wa Syria Bashar al Assad,licha ya vita vya kutaka kuiangusha serikali,Adam Szubin ameambia BBC.
IS imeiba takriban dola bilioni moja kutoka maeneo inayodhibiti.
Muungano
unaoongozwa na Marekani umekuwa ukishambulia maeneo ya kundi hilo
ikiwemo maeneo ya mafuta nchini Syria na Iraq kwa zaidi ya mwaka mmoja
sasa.
No comments:
Post a Comment