Wednesday, December 30, 2015


Umoja  wa  Afrika  leo  umetishia  kuyawekea vikwazo makundi  hasimu  nchini  Burundi  iwapo  yatashindwa kuhudhuria  mazungumzo  ya  amani  mwezi  ujao, wakati ukiibana  serikali   kukubali jeshi  la  kulinda  amani.
Serikali  ya  Burundi  na  upinzani, pande  zilizokutana nchini  Uganda  siku  ya  Jumatatu,  zinatarajiwa  kukutana tena  Januari  katika  mji  wa  kaskazini  mwa  Tanzania  wa Arusha kwa  mazungumzo  yenye  lengo  la  kumaliza miezi  kadhaa  ya  ghasia.
Ghasi  hizo  zimeongeza  hofu  ya  kurejewa  kwa  vita kamili  katika  taifa  hilo  dogo  la  Afrika  ya  kati, miaka tisa baada  ya  kumalizika  kwa  vita  vya  wenyewe  kwa wenyewe. Maafisa  wa  Uganda  wamesema  mazungumzo yataanza  tena  Januari  6  lakini  ujumbe  wa  serikali  ya Burundi  umesema  hakuna  muafaka  uliofikiwa  kuhusiana na  tarehe  ya  mkutano  huo.
Rais  wa  halmashauri  ya  Umoja  wa  Afrika  Nkosazana Dlamini-Zuma ameonya  kuhusu  vikwazo  hivyo  iwapo ghasia  zitaendelea  na  mazungumzo hayatafanyika.

No comments:

Post a Comment