Wednesday, December 30, 2015


Waziri  mkuu  wa  Iraq Haider al-Abadi  jana  alifanya  ziara katika  mji  uliokombolewa  wa  Ramadi, baada  ya  majeshi ya  serikali  kutangaza  kuukomboa  mji  huo  kutoka  kwa kundi  la  Dola  la  Kiislamu, na  kupata  ushindi  muhimu.
Abadi  aliwasili  kwa  helikopta  katika  mji  huo  ulioharibiwa kwa  vita, ambao  uko  kilometa 100 magharibi  ya  mji mkuu  Baghdad  na  ni  mji  mkuu  wa  jimbo  la  Anbar.
Waziri  mkuu ameapa  siku  ya  Jumatatu , baada  ya majeshi  yanayopambana  na  magaidi  kupandisha bendera  ya  taifa  katika  majengo  ya  serikali  mjini Ramadi kwamba atawaondoa  wanamgambo  wa  IS kutoka  nchi  hiyo  ifikapo mwishoni  mwa  mwaka  2016.
Ni  jambo  la  kawaida  kwa  waziri  mkuu  kutembelea  miji iliyokombolewa  lakini  amefurahishwa  mno na  ushindi katika  mji  wa  Ramadi, mji  ambao  majeshi  ya  serikali yaliupoteza  Mei mwaka  huu.

No comments:

Post a Comment