Friday, December 11, 2015

Mawaziri wa Rais MAGUFULI walivyojadiliwa na UVCCM leo, kuna msisitizo wa haya mawili..


Jana Rais wa Tanzania John Magufuli alitangaza Baraza jipya la Mawaziri, likiwa na jumla ya Wizara 18 pamoja na Mawaziri 19.
Wadau wengi nchini wametoa maoni yao kuhusu uteuzi huo wakiwemo Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi UVCCM.
Katika maoni yao UVCCM kupitia kwa Katibu wa Idara ya Uhamasishaji Egla Obed wamempongeza Rais kwa uteuzi mahiri na makini wa Baraza hilo ambalo ni dogo lakini limekamilika katika kuhakikisha linagusa kila sekta na kuhakikisha linapunguza na kubana matumizi yasiyo ya lazima.
Kuhusu uteuzi wa Mawaziri wengi vijana, UVCCM amesema haya >>> “Tumeridhishwa na uteuzi huu ambao umesheheni mawaziri na Manaibu wenye uwezo na weledi mkubwa sana, hatuna mashaka kwamba watafanya kazi kwa kasi na uzalendo, tumefarijika zaidi kwa kuwa lina vijana wengi ambao ni nguvu kazi ya Taifa, tunaiona dhamira ya dhati ya Rais kuhakikisha Tanzania inapata mabadiliko ya haraka” >>> Egla Obed.
Na kuhusu  ishu kazi na kasi ya Rais Magufuli je? Majibu yao ni haya >>Serikali itimize wajibu wake wa kuhakikisha inawawezesha wananchi kiuchumi na Mawaziri wana kazi kubwa ya kuhakikisha wanaendeleza mapambano ya kubana matumizi yasiyo ya lazima ili fedha zielekezwe kwenye kuboresha huduma za kijamii, Watanzania hatatuwaelewa Mawaziri wetu kama hawatofuata maagizo ya Chama yaliyoanza kutekelezwa kwa kasi na Rais” >>> Egla Obed.

No comments:

Post a Comment