Wednesday, December 30, 2015

Image result for IS
Marekani  imesema  kiongozi wa  Dola  la  Kiislamu Mfaransa , ambaye  alihusika  katika  mashambulizi  ya mjini  Paris, ameuwawa  katika  mashambulizi  ya  anga  ya muungano  unaoongozwa  na  Marekani.
Charaffe al-Mouadan, ambaye  aliwasiliana  na  aliyedaiwa kuwa  kiongozi  wa  mauaji  katika  mji  mkuu  wa  Ufaransa Paris, ameuwawa  wakati  wa  shambulio  la  anga Desemba  24  mwaka  huu.
Wizara  ya  ulinzi  ya  Marekani  imesema  alikuwa  mmoja wa  viongozi 10  wa  juu  wa  IS waliouwawa  katika  muda wa miezi  michache iliyopita kwa  mashambulizi  ya  ndege zisizokuwa  na  rubani.

No comments:

Post a Comment