Magufuli afanya ziara ya kushtukiza Hazina Kuu.
Rais mpya wa Tanzania John Magufuli leo amefanya ziara ya kushtukiza katika Hazina Kuu siku moja tu
baada yake kuapishwa.
Rais huyo amefanya ziara hiyo fupi kutoka ikulu muda mfupi baada ya kumuapisha Mwanasheria Mkuu George Mcheche Masaju.
Bw Masaju aliteuliwa mara ya kwanza kuwa Mwanasheria
Mkuu na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Januari mwaka huu baada ya
kujiuzulu kwa George Werema.
Bw Magufuli hakuzungumza rasmi na wanahabari baada ya kumaliza ziara hiyo.
Hata
hivyo, mwandishi wa BBC Tulanana Bohela anasema kuna uwezekano
amezungumza na maafisa wa hazina kuu kuhusu hali ya mikopo ya wanafunzi.
Wakati wa kampeni, Bw Magufuli aliahidi kufanya elimu kuwa bila malipo kuanzia shule za msingi hadi shule za sekondari.
Taarifa
kutoka ikulu ya Dar es Salaam zinasema kwenye mkutano na maafisa wakuu
wa Wizara ya Fedha, Bw Magufuli aliwaagiza kuziba mianya yote
inayotumiwa na wakwepa kodi.
No comments:
Post a Comment