Monday, November 9, 2015

Mkurugenzi wa MTN ajiuzulu kufuatia faini Nigeria





 Mkurugenzi wa MTN ajiuzulu kufuatia faini Nigeria



Mkurugenzi mkuu wa kampuni ya simu ya MTN amejiuzulu kufuatia faini kubwa ya dola bilioni 5.2 iliyotozwa na Nigeria
Mkuu huyo wa kampuni hiyo kubwa zaidi barani Afrika Sifiso Dabengwa,aliwasilisha barua ya kujiuzulu mara moja kwa maslahi ya wenye hisa na uendelevu wa kampuni hiyo.
Faini hiyo iliyotozwa na tume ya mawasiliano ya Nigeria kufuatia utepetevu wa MTN ya kukataa kuzima nambari za simu ambazo hazijasajiliwa kwa mujibu wa kanuni mpya za taifa hilo.
MTN ilipewa majuma mawili pekee kuwa imelipa faini hiyo kubwa inayotoshana na faida iliyopata mwaka uliopita.
MTN ina hadi tarehe 16 Novemba kuwa imelipa faini hiyo ya dola 5.2.
Dabengwa aliandika ''kufuatia faini kubwa iliyotozwa MTN Nigeria ,kwa niaba yangu na wenye hisa wa kampuni hii nimeamua kujiuzulu mara moja''
Dabengwa amekuwa mkurugenzi wa kampuni hiyo tangu mwaka wa 2011.
Phuthuma Nhleko amechaguliwa kuwa kaimu mkurugenzi wa kampuni hiyo kwa kipindi kisichozidi miezi 6.
MTN ina hadi tarehe 16 Novemba kuwa imelipa faini hiyo ya dola 5.2. 
 

 
Inadhaniwa kuwa serikali ya Nigeria ilichukua hatua kali za kinidhamu dhidi ya MTN kufuatia utekaji nyara wa aliyekuwa waziri wa zamani wa fedha Chifu Olu Falae.
Waliomteka nyara walitumia simu ambayo haijasajiliwa ya MTN kuitisha malipo ya kumkomboa Nigeria ndio mteja mkubwa zaidi wa kampuni hiyo yenye asili ya Afrika Kusini ikiwa na wateja milioni 28.5.
Soko la pili kwa ukubwa kwa MTN ni Iran na kisha Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment