Mlipuko chanzo ajali ya ndege, nchini uingereza.
Haya ndiyo mabaki ya ndege ya Urusi ililyoanguka Misri
Uingereza imetoa
angalizo kwamba huenda mlipuko ndio uliosababisha ndege ya shirika la
ndege la Urusi kuangukia nchini Misri na kuua abiria wote mia mbili na
ishirini na wanne waliokuwa kwenye ndege hiyo.
Safari za ndege
kati ya nchi za Misri na Uingereza na pwani ya mapumziko ya rasi ya
Sharm el-Sheikh zimesitishwa kama tahadhari wakati maofisa kutoka nchini
Uingereza wakiendelea kuangalia hali ya usalama katika uwanja wa ndege.Halikadhalika safari za kutoka na kuingia katika rasi hiyo zimesitishwa na Ireland.
Mamlaka ya safari za anga nchini Urusi hivi karibuni walitoa tahadhari kuwa ni mapema mno kuhisi nini chanzo cha ajali hiyo.
Mabaki ya ndege hiyo na kisanduku cheusi chenye kurekodi mwenendo wa ndege hiyo bado vinafanyiwa uchunguzi.
Mpaka sasa kundi la wanamgambo wa kiislamu, la Islamic State limereudia kukiri kuwa linahusika na ajali hiyo.
No comments:
Post a Comment