Wednesday, November 4, 2015

Majeshi ya upinzani yateka eneo Syria


Wizara ya ulinzi ya Marekani imesema kwamba wanajeshi wa upinzani waliounda kundi lao hivi karibuni nchini Syria,wamefanikiwa kutwaa eneo lenye ukubwa wa kilomita mia mbili katika mapambano yake na kikundi cha kigaidi cha Islamic State upande wa kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.
Msemaji wa wizara hiyo ya ulinzi aliyeko mjini Baghdad,Steve Warren,ameelezea kuwa mapambano hayo yanayoendelea karibu na mji wa Al-Hawl yanahusisha maelfu ya wapiganaji wa upande wa upinzani ambao wameongezewa nguvu na askari wa angani wa majeshi washirika ya Marekani.
Kikundi hicho kinachojiita jeshi la Syria lenye muungano wa nchi za Kiarab,kimekuwa kikitoa ahadi ambapo mpango mpya wa nchi ya Marekani wenye lengo la kupambana na kikundi hicho cha wanamgambo wa Islamic State walioko nchini Syria.

No comments:

Post a Comment