Huu ni mpango wa Wema Sepetu kwa mwaka 2016
Mwaka 2015 unakaribia kuisha na baadhi ya watu wameshaanza kufanya
mipango yao kwa mwaka 2016. Kwa mwaka 2015 Wema Sepetu ametajwa mara
kadhaa kutokua na maelewano na baadhi ya marafiki zake wa zamani kama
Kajala, pia kuendeleza uhusiano mzuri na watu aliokua hapatani nao
zamani kama Penny.
Kwenye moja ya mipango ya Wema Sepetu kwa mwaka 2016 ameweka wazi
kwamba yeye hana mpango wa kuanza mwaka akiwa na beef na mtu yoyote.
Wema amesisitiza kwamba anaomba watu wote aliowakosea kwa mwaka 2015
wamsamehe na yeye anawasamehe wote waliomkosea.
Maneno ya Wema Sepetu kuhusu mpango huo yapo hivi, “Mi nataka
mwaka unapoanza inshallah tukijaaliwa nisiwe na beef na mtu yoyote wala
kiumbe yoyote… Kwa wale nilowakosea na walionikosea …. Nasema Im
sorry….. Life Goes On…. We all live to make mistakes…. Ama nene…. And I thank everyone for making me the person Iam TODAY….”
No comments:
Post a Comment