Kumbe Justin Bieber bado anampenda Selena Gomez, kazungumza haya kwenye jarida la Billboard.
Zikiwa zimebaki siku chache tu mpaka msanii wa muziki wa Pop kutoka Marekani, Justin Bieber aisogeze kwetu Album yake ya kwanza ndani ya miaka mitatu, Purpose, msanii huyo amepata shavu la kuonekana kwenye toleo jipya la jarida la Billboard la Marekani.
Muimbaji huyo mwenye umri wa miaka 21
amezungumzia vitu vingi kwenye jarida hilo ikiwemo kuvuja kwa picha zake
za utupu, mpenzi wake wa zamani Selena gomez na mtazamo wake kuhusu umaarufu wa wadogo zake Kim kardashian, Kylie Jenner na Kendel Jenner.
Kuhusiana na kuvuja kwa picha zake za utupu ambazo zilipigwa bila ridhaa yake mwenyewe, Justin Bieber ameliambia jarida la Billboard kuwa kitendo cha picha zile kupigwa na baba yake ilikuwa ni uvamizi wa maisha binafsi, japo baba ni baba…
>>> “ Ile
picha kupigwa ilikuwa ni kitendo kinachoingilia maisha yangu binafsi.
Niliona nimedhalilishwa kwa hali ya juu, lakini baba yangu aliniambia
nisiichukulie serious. Badaae nikaona kama kichekesho tu… Nilikuwa
naogopa, na hapo mwanzoni nilipoiona ilikuwa imeniziba kwa nyuma,
nilisema Yesu wangu ni nini hiki…” <<< Justin Bieber.
Kuhusiana na Mpenzi wake wa zamani Selena Gomez, Justin Bieber
amesema anajivunia kuona mafanikio yake makubwa kwa sasa, na amedai
kuwa unapompenda mtu hata kitu kikija kati yenu upendo ulionao juu ya
mtu huyo utabaki pale pale…
>>> “ Najivunia
sana kumuona jinsi alivyokua mpaka kufikia hii leo… ukimpenda mtu kwa
kiasi hiki hata kije nini kati yenu upendo mlionao kati yenu hauwezi
kufa…” <<< Justin Bieber.
Hapa chini nimezisogeza kwako baadhi ya picha alizopiga Justin Bieber kwenye cover shoot ya jarida la Billboard.
No comments:
Post a Comment