Friday, November 6, 2015

Obama atoa onyo kali kwa Afrika Kusini


Rais wa Marekani Barack Obama ameipa Afrika ya Kusini siku 60 kuondoa vikwazo katika bidhaa za kilimo kutoka Marekani la sivyo ataiondolea msamaha wa kodi wa bidhaa.
Mpango huo utaathiri karibu robo ya billion ya dollar ya bidhaa za Afrika kusini zinazosafirishwa nchini Marekani.
Obama amechukua hatua hiyo kwa vile Afrika Kusini imeendelea kuweka vikwazo kwa wafanyabiashara wa Marekani.
Afrika Kusini ilipiga marufuku kuagiza mazao ya kuku mwezi Decemba kutokana na kutokea kwa mlipuko wa ugonjwa wa mafua ya ndege na kwa miaka kadhaa imekuwa ikitoa adhabu ya kodi kwa baadhi ya bidhaa za kuku kutoka Marekani.

No comments:

Post a Comment