Tuesday, November 10, 2015

Wapenzi wa jinsia moja watoroka Uganda

 Vijikaratasi vilivyochapishwa katika kuta



Mamia ya watu wa jamii ya jinsia moja nchini Uganda wamelitoroka taifa hilo ili kukwepa ubaguzi na mateso.
Lakini sasa wamekwama nchini Kenya ambapo hali sio shwari.
Mwandishi wa BBC Emmanuel Igunza alisafiri hadi katika kambi moja ya wakimbizi ambapo vijikaratasi vilichapishwa katika kuta vikiwataka wakaazi kutojichanganya na watu wa jinsia hiyo.
Raia hao wa Uganda wamepiga kambi huko Kakuma kutoka taifa lenye amani.
Wakaazi wengine waliopo katika kambi hiyo wanatoka katika maeneo yaliyokumbwa na migogoro kama vile Sudan Kusini na Somalia.

No comments:

Post a Comment