Wednesday, December 2, 2015

Huduma ya taifa' Eritrea ni dhalimu

 Huduma ya jeshi ni lazima kwa raia wa Eritrea
Raia wengi wa Eritrea wamekimbia nchi kuepuka huduma ya jeshi
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu Amnesty International, limetaka jamii ya kimataifa kutambua shughuli ya serikali ya Eritrea kuwaigiza raia wake kwa nguvu katika huduma ya tiafa, kama ukiukaji wa haki za binadamu.
Shirika hili linasema hatua hii ya serikali inachochea tatizo la ongezeko la wakimbizi duniani.
Kwenye ripoti yake, Amnesty International inasema maelfu ya vijana wa Eritrea wanaikimbia nchi na kutafuta hifadhi Ulaya ili kuepuka kuingizwa kwenye huduma ya taifa.
Huduma hii imetajwa kama inayojumuisha ajira ya lazima, huku makurutu wengi wakisalia kufanya shughuli kinyume na zile za kijeshi kama vile kilimo na ujenzi.
Baadhi ya raia wa Eritrea waliokimbia nchini waliambia shirika hilo kwamba waliojaribu kukimbia kutoka huduma hiyo hupata adhabu kali.
Eritrea imejitetea dhidi ya madai kwamba inatumia huduma hii kuwadhulumu raia wake na kusema wakosoaji wa mpango huo wanaingilia uhuru wake na kuhujumu maendeleo.

No comments:

Post a Comment